• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Helium Yaibuka Kikao cha Bodi ya Barabara na kuibua gumzo.

imewekwa Tar: February 25th, 2021

Wajumbe wa Bodi ya Barabara Mkoani Rukwa wamesikitishwa na kitendo cha Wakala wa Barabara za Mijini na Vijini (TARURA) Pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD) kushindwa kuonyesha mpango wa kufungua barabara zinazoelekea ziwa Rukwa hasa katika maeneo ambayo utafiti unaonesha kuwa kuna gesi ya Helium inayoweza kuchimbwa.

Akiibua hoja hiyo katika kikao cha Bodi hiyo Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Ya Wilaya ya Sumbawanga Mh. Apolinary Macheta alisema kuwa hapo awali katika bonde la Ziwa Rukwa kulikuwa na njia za kuelekea katika ziwa Rukwa lakini hivi sasa hakuna na hivyo kuiomba serikali kuona umuhimu wa kutenga bajeti kwaajili ya kuweka miundombinu Rafiki kwaajili ya kufika katika mradi huo wa helium.  

“Lakini Mheshimiwa Mwenyekiti ukiangalia kuanzia (Kijiji cha) Muze, Uzia – Kijiji kimoja kutoka Muze, kama nilivyosema zamani kulikuwa na njia magari yanaweza yakaingia huko ziwani, (lakini sasa) hakuna hata njia moja, hivyo nadhani jambo hili tulione kwa kina sana,” Alisema.

Akichangia hoja hiyo mbunge wa Nkasi Kaskazini Mh. Aida Khenan alisema kuwa haiwezekani kuifikia gesi hiyo endapo miundombinu sio rafiki na hivyo kutoa kutoa ushauri kwa TARURA juu ya kuweka vipaumbele vya ujenzi wa barabara ambazo zitachochea ukuaji wa uchumi wa Mkoa wa Rukwa.

“Tunazungumzia (mkoa) Songwe, wanaichukua hiyo fursa kwa maana gani, kama wameona sisi hatusemi lazima wafanye hivyo na mwisho wa siku wataanza kunufaika Songwe badala ya Rukwa, nilikuwa nashauri tena Pamoja na kwamba kuna brabara ambazo ni korofi sana, lakini lazima tuangalie kwanini tupeleke fedha pale, tunapeleka pale kwasababu barabara hii ikikamilika, vichocheo vya uchumi vinavyopita kwenye hii barabara vinaweza kutengeneza barabara nyingine,” Alisema.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kwela Mh. Deus Sangu alishauri bajeti ya TARURA kuwa na fungu la kuwezesha kujenga barabara zinazoelekea katika ziwa Rukwa kutokana na umuhimu na uharaka wake na kuiwasilisha Wizarani na hivyo ngazi ya mkoa kujivua lawama na kulibakisha mikononi mwa wizara husika na wenye maamuzi.

“Niwaombe TARURA mwaka huu wa fedha uwe ni mwaka wa mwisho kuwa na ‘Template’ ya aina hii (ya bajeti) tubadilishe mkafanye ‘survey’ mpya ya barabara, mje na mahitaji yaliyo halisi, tupeleke mahitaji yaliyo halisi siyo kukariri mambo ya miaka ya 2007 kwamaba milioni 600 ndio ‘Ceiling’ mwengine ana Shilingi bilioni 1.5 hatutafika,” Alieleza.

Katika kukazia hilo Mwenyekiti wa Bodi hiyo ambaye pia ni Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alisema kuwa Mkoa wa Rukwa umejaaliwa kuwa na rasilimali kubwa ya gesi ya Helium na endapo miundombinu ya kufikia gesi hiyo sio Rafiki, wawekezaji watashindwa kufika katika maeneo hayo.

“Ni lazima barabara hizi zipitike na kwa namna ile ni lazima zipate fedha za kutosha kutoka wizara inayohusika, vinginevyo tutakuwa tunazungumza tu ‘Helium gas’ umuhimu wake lakini hatuwezi kuichima ile gesi kwasababu ya barabara, kwahiyo ni lazima TANROAD na TARURA waongeze bajeti ya barabara zao, hususan kwenye bonde la ziwa Rukwa ili hiyo ‘Helium gas’ tuweze kuizungumzia vizuri katika kuichimba na kuitangaza, hatuwezi kuitangaza kama wawekezaji hawawezi kufika kwasababu ya kutokuwepo kwa barabara,” Alisisitiza.

Kwa mwaka wa fedha 2021/2022 TARURA wameomba kupitishiwa bajeti ya Shilingi 38,544,061,553.75 kwaajili ya matengenezo ya barabara ikijumuisha fedha za matengenezo Shilingi, 4,119,774,160.83 na Shilingi 34,424,287,392.92 kwaajili ya miradi ya maendeleo kwa barabara zenye urefu wa km 450.37 kwa matengenezo ya barabara na vivuko mchanganyiko 51.

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • UTARATIBU WA UOMBAJI WA VITAMBULISHO VYA UJASILIAMALI March 24, 2021
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara waombwa kuwa na huruma na wanaofunga mwezi wa Ramadhan

    April 16, 2021
  • Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

    April 15, 2021
  • Mwamko mdogo wa Wananchi wakwamisha zoezi la Urasimishaji Makazi Sumbawanga

    April 14, 2021
  • Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

    April 05, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa