• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mapato ya Manispaa ya Sumbawanga kupaa kwa 46% kutokana na ujenzi Stendi ya Kisasa.

imewekwa Tar: May 7th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amepongeza juhudi zinazofanwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga katika kukusanya mapato pamoja na kuwa mbunifu wa kuongeza vyanzo mbalimbali vya mapato ili kuweza kutatua na kukamilisha miradi mbali mbali ya manispaa hiyo.

Amesema kuwa kukamilika kwa stendi hiyo ya kisasa kutaongeza ukusanyaji wa mapato wa karibu asilimia 46 ya mapato ya sasa ambapo manispaa hiyo ilikisia kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019 ikusanye shilingi 2,212,104,000 na hadi kufikia mwezi machi 2019 ilikuwa imekusanya shilingi 2,424,032,802.71 ambayo ni sawa na asilimia 110 ya makusanyo.

“Hii stendi ikimalizika mapato ya kutoka hapa itakuwa bilioni 1, sasa hii ni karibu asilimia 46 ya mapato yote ya manispaa kwa sasa hivi, hamuoni kwamba mapato ya manispaa yataongezeka kwa kasi kubwa sana na kwa hali hiyo hata waheshimiwa madiwani wataweza kutekeleza mipango yao vizuri na kwa ukamilifu sana na watakaonufaika ni sisi wananchi wote ndani ya Manispaa, “Alisema.

RC Wangabo ametoa kauli hiyo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa ujenzi wa kituo kipya cha kisasa cha mabasi kitakachojengwa katika eneo la Katumba azimio lililopo kilomita 12 kutoka Sumbawanga mjini, ambapo mradi huo ukikamilika utaiingizia manispaa ya Sumbawanga Shilingi 1,027,800,000 kwa mwaka.

Aidha, Aliwataka wakurugenzi wa halmashauri nyingine za mkoa huo kuipa kipaumbele miradi ya kimkakati, miradi ambayo huleta fedha nyingi kwa wakati mmoja kwani kwa kufanya kutazifanya halmashauri hizo kuweza kutatua kero nyingi za wananchi pamoja na kuboresha huduma mbalimbali za kijamii kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga James Mtalitinya alisema kuwa miundombinu itakayojengwa katika eneo hilo ni pamoja na Eneo la kuegeshea mabasi ya ndani na nje ya mkoa, bajaji, bodaboda, taksi na baiskeli, vyumba vya maduka, jengo la utawala, kituo kidogo cha polisi, mama lishe, choo cha kulipia, uzio, Taa, mifereji, vyumba kwaajili ya benki na ATM’s na vyumba vya mazoezi (Gyms)

“Mzabuni aliyepatikana kwaajili ya ujenzi wa kituo cha Kisasa cha Mabasi Katumba azimio ni Sumry Enterprises Ltd. Eneo ambalo litatumika kwaajili ya Ujenzi wa Stendi ni ekari 10 na ekari 12 zitakuwa ni kwaajili ya mipango ya halmashauri ya hapo baadae. Mradi huu ni chanzo cha mapato ambacho kitaweza kutuingizia fedha itakayotumika kujenga au kumalizia miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo ndani ya Manispaa na Kuboresha huduma mbalimbali.” Alisema.   

Kwa mwaka wa fedha 2018/2019 Manispaa ya Sumbawanga iliweka bajeti ya ujenzi wa kituo cha kisasa cha mabasi Katumba Azimio kupitia fedha za Mradi wa Uimarishaji miji (ULGSP) na kumpata mkandarasi Sumry Enterprises Ltd ambaye atahusika na ujenzi huo utakaogharimu shilingi 5,955,363,986 bila ya VAT

 

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza Mkoa wa Rukwa 2018 January 05, 2018
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Kikao cha Road Board Mkoani Rukwa October 08, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Utoro, Uvivu na kutoshirikisha wazazi kwatajwa kuwa kikwazo cha ufaulu Rukwa.

    December 06, 2019
  • Mawakala wa Mbolea watolewa wasiwasi huku wakulima wakikataa rangi ya mbolea Inbox x

    December 03, 2019
  • Wanarukwa wahamasishwa kulima kwa tija ili kujiongezea kipato

    December 02, 2019
  • TARURA watakiwa kushughulikia maeneo korofi msimu wa mvua

    November 30, 2019
  • Angalia Zote

Video

Kisa Kamili cha Mama Mjamzito Kujijeruhi tumboni chafafanuliwa na RMO Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa