• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Milioni 151 zatumika kuongeza nguvu ya kupambana na Ukimwi Rukwa.

imewekwa Tar: October 31st, 2018

Ofisi ya mkuu wa mkoa wa Rukwa kwa kushirikiana na mradi wa Military HIV Research Program (MHRP) umetumia Shilingi 151,109,042 kununua gari aina ya Land Cruiser Hardtop kwaajili ya shughuli zinazohusiana na mapambano dhidi ya Ukimwi.

Gari hiyo ambayo alikabidhiwa kwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Bw.Msongela Palela na mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo imenunuliwa kutokana na fedha zilizovuka mwaka 2016/2017 ikiwa ni makubaliano baina ya katibu tawala na mradi juu ya fedha zilizovuka mwaka kupangiwa matumizi yanayolenga kuboresha huduma za Ukimwi.

Wakati akikabidhi gari hiyo Mh. Wangabo alitahadharisha matumizi ya gari hiyo huku akipiga mfano wa gari ya Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF) ya halmashauri ya Wilaya ya Kalmabo iliyokuwa na mazoea ya kwenda kwenye sehemu za starehe kuwa mshauri wa mradi huo tayari ameshachukuliwa hatua za kinidhamu.

“Tarehe 7 mwezi wa 10 gari hii tulilishika hapa Sumbawanga likiwa eneo la starehe na huyo mshauri wa mradi huo ndiye aliyekuwa anaendesha gari hilo, tulichukua hatua kali za kumuondoa na kumrudisha kwa mwajiri wake kwaajili ya hatua nyingine za kinidhamu, nitoe wito kwa madereva wa serikali kutumia magari kwa mambo yao binafsi, suala hili lisijitokeze, hatua kali zitachukuliwa,” alisisitiza.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkurugenzi wa mradi huo Bw. Riziki Kasimu ameshukuru ushirikiano anaoupata kutoka katika halmashauri na serikali ya Mkoa ili kuhakikisha wanashusha na kutokomeza maambukizi ya Ukimwi na ameiomba serikali ya Mkoa wa Rukwa kutoa kipaumbele kwa kazi za Ukimwi katika matumizi ya gari.

“Pamoja na Kazi zote zilizopo Mkoani, tungependa kazi za mradi zipewe kipaumbele katika matumizi ya gari, ni kweli kwamba tuna kazi nyingi ama majukumu mengi ambayo hayo magari yangepaswa kufanya na sisi kama washirika kwenye maendeleo hatuwezi kusema gari hili litumike moja kwa moja kwa Ukimwi tu, lakini pale tunapokuwa na majukumu ya msingi ya Ukimwi tungependa msisitizo utolewe huko,”Alisema.

Mtadi huo tayari umeshatoa gari 7 katika Mkoa wa Rukwa, 4 katika Halmashauri zote za Mkoa na 3 katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa jambo lililosaidia kurahisisha shughuli za kupambana na maambukizi ya Ukimbwi na hatimae kushuka kutoka asilimia 6.2 mwaka 2015 hadi asilimia 4.4 mwaka 2018.

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Madiwani wilayani Kalambo waapa kumaliza upungufu wa vyumba vya madarasa

    January 07, 2021
  • Ukaguzi wa Dawa kwenye vituo vya kutolea Huduma – Rukwa

    January 06, 2021
  • NASIBU WAZIRI AKIRI KUWEPO CHANGAMOTO BIMA YA MFUKO WA AFYA YA JAMII

    January 05, 2021
  • RC Wangabo awaonesha wananchi njia ya kupata kipato kikubwa kwa nguvu ndogo kwa mwaka 2021.

    January 01, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa