• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo atembelea kituo cha Afya na kukuta madudu

imewekwa Tar: November 6th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza mkurugenzi wa halmasshauri ya Wilaya ya Kalambo kuhakikisha anampatia taarifa ya kila wiki juu ya maendeleo ya ujenzi wa kituo cha afya cha Kanyezi, kilichopo kata ya Kanyezi wilayani Kalambo.

Maesema kuwa tangu kuanza kwa miradi ya upanuzi na ujenzi wa vituo vya afya katika halmashauri hiyo kumekuwa na ubabaishaji hasa wa kuchelewa kununua vifaa vya ujenzi pamoja na malipo kwa mafundi ambapo ujenzi huo unatumia mfumo wa “Force Account” kutekeleza kazi hiyo.

“Sasa wewe afisa mipango, Mkurugenzi, kuanzia sasa hivi nataka muwe mnanipa taarifa “on weekly basis” (za kila wiki) kwamba nini kinachoendelea katika ujenzi huu, nisingependa tabia hii ya kusua sua iendelee, muiache mara moja, mnaumiza hawa wajenzi, halafu hamuwezi kuwalipa fidia, ingekuwa hawatimizi wajibu wao ingekuwa kitu kingine, kama ilivyotokea kule Kijiji cha Legeza mwendo fundi akakimbia ni kwasababu ya namna hii ubabaishaji wa malipo, mjipange,” Alisisitiza.

Aliyasema hayo alipofanya ziara ya kushtukiza katika kuangalia maendeleo ya ujenzi wa kituo hicho cha afya ambacho kimepandishwa hadhi kutoka kuwa zahanati ya kijiji cha Kanyezi na kukuta zimebaki siku 15 kutakiwa kukabidhi majengo hayo lakini bado wapo katika hatua ya linta.

Kwa upande wake Afisa Mipango wa halmashauri hiyo Bw. Erick Kayombo aliahidi kuwa pamoja na kucheleweshewa kupata fedha lakini halmashauri tayari imeshaagiza vifaa vyote vinavyotakiwa kwaajili ya kumalizia ujenzi.

Kauli hiyo ya Mh. Wangabo ilikuja baada ya mmoja wa mafundi wadogo bw. Hamisi Pesambili kumlalamikia Mkuu wa Mkoa juu ya kucheleweshewa vifaa kwaajili ya kuendelea na ujenzi hali inayowafanya waishi kwa taabu huku wakiwa wameacha familia zao mjini sumbawanga na kwa siku kulipwa shilingi 10,000 fedha ambayo hawaridhiki nayo.

Katika kulirekebisha hilo, Mh. Wangabo alimuagiza mhandisi wa Halmashauri ambaye pia ni msimamizi wa jengo hilo kuhakikisha kuwa wanasimamia malipo ya mafundi wadogo kutoka kwa mafundi wao na sio kuishia kuwalipa mafundi huku hawajui kama vibarua hao wanalipwa kama walivyokubaliana na mafundi wao na kuongeza kuwa kutolipwa vizuri kwa vibarua kunaweza kupelekea majengo kutokuwa na ubora unaotarajiwa.

Serikali ya awamu ya tano imefanikiwa kujenga vituo vitatu vya afya katika halmashauri ya Wilaya ya Kalambo na kutumia zaidi ya shilingi bilioni moja kwaajili ya ujenzi na utanuzi huo huku ikielekeza shilingi bilioni 1.5 kwaajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya.

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • UTARATIBU WA UOMBAJI WA VITAMBULISHO VYA UJASILIAMALI March 24, 2021
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara waombwa kuwa na huruma na wanaofunga mwezi wa Ramadhan

    April 16, 2021
  • Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

    April 15, 2021
  • Mwamko mdogo wa Wananchi wakwamisha zoezi la Urasimishaji Makazi Sumbawanga

    April 14, 2021
  • Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

    April 05, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa