• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wahitimu wa chuo cha NDF waelezwa fursa za uwekezaji zinazopatikana Rukwa

imewekwa Tar: January 7th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amefafanua fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika Mkoa hasa sekta ya kilimo kwa wahitimu wa mafunzo kwa vitendo kutoka katika Chuo cha Taifa cha Ulinzi waliotembelea mkoani hapa ili kujionea maendeleo ya mkoa.

Wahitimu hao kutoka katika nchi kadhaa barani Afrika wamelenga kutembelea katika viwanda vikubwa vinavypoaptikana katika mkoa, maeneo ya uwekezaji wa kilimo, kufika kwenye vivutio vya utalii, machimbo ya makaa ya mawe pamoja na hifadhi za misitu.

Mh.Wangabo alisema kuwa uwekezaji wa kwenye viwanda unahitajika kwasababu ya uwepo wa mazao ya kulisha viwanda hivyo ikiwemo viwanda vya kuchakata mahindi, maharage na mpunga na kuwaondoa shaka juu ya upatikanaji wa umeme kwani hadi kufikia mwaka 2020 vijiji vyote vya mkoa wa Rukwa vitakuwa na umeme.

“Maeneo mazuri ya uwekezaji upo kwenye viwanda hasa viwanda vya kuchakata mazao ndani ya mkoa wetu, pia mwaka huu tuna zao la alizeti kama zao la Kimkakati ambapo hadi sasa kuna tani za mbegu zaidi ya 11,000 ambazo zimeshanunuliwa na wakulima na kupandwa na hivyo tunategemea uzalishaji mkubwa wa alizeti kwa mwaka huu na hivyo tunawaalika wawekezaji kuweka viwanda vya uchakataji wa alizeti ikiwa ni zao la kimkakati kwenye mkoa wetu.” Alisema.

Aidha, alibainisha kuwa katika kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano, mkoa umejipanga kulima zao la kahawa ambalo ni moja ya mazao matano ya kimkakati kwa serikali, na kusisitiza kuwa upatikanaji wa samaki katika ziwa Tanganyika na ziwa Rukwa bado unahitaji uwekezaji ili kukuza sekta hiyo na hatimae kukuza vipato vya wavuvi wa maeneo ya maziwa hayo, huku akielezea uboreshwaji wa miundombinu ya barabara na kiwanja cha ndege cha mkoa. 

Ameyasema hayo wakati akijibu swali la Brigedia Generali Mohamed Montaser muhitimu kutoka nchini Misri aliyetaka kujua maeneo ya vipaumbele katika uwekezaji kwa mkoa wa Rukwa.

Halikadhalika, Kiongozi wa wahitimu hao Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza SACP Justine Kaziulaya aliushukuru uongozi wa Mkoa wa Rukwa kwa mapokezi mazuri waliyoyapata na kuomba kupokewa tena endapo watarudi Mkoa wa Rukwa katika miaka inayofuata.

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wananchi wasisitizwa kuitumia wiki ya sheria kama fursa ya mafunzo ya bure ya sheria.

    January 24, 2021
  • MABARAZA YA ARDHI YATAJWA KUWA CHANZO CHA MIGOGORO

    January 23, 2021
  • Kamati ya Amani Rukwa yamuomba RC kufikisha salamu zao kwa Rais Magufuli.

    January 22, 2021
  • Kijiji kitakachokaribisha “Lambalamba” Kuwekwa chini ya Ulinzi

    January 21, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa