Mradi wa upimaji viwanja Nambogo na Katumba Azimio umetekelezwa kwa ubia kati ya Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga na Mfuko wa Mafao ya Kustaafu (GEPF), hii itasaidia upatikanaji wa viwanja vilivyopimwa na kuwekewa miundombinu ya msingi na kusogeza huduma mbalimbali kwa wananchi waishio katika kata za pembezoni za Pito, Molo, Milanzi, Lwiche nk.
LENGO LA MRADI
Lengo kuu la mradi huu wa Nambogo ni kuwa na mji wa kisasa utakaokuwa na huduma mbalimbali ili kupunguza msongamano wa kufuata huduma katika eneo la kitovu cha mji (Central Business District) kwa siku za usoni. Sambamba na hilo, mradi utasaidia kuongeza upatikanaji wa viwanja vilivyopimwa na kuwekewa miundo mbinu ya msingi, hivyo kupunguza kasi ya ujenzi holela.
HALI HALISI YA UPIMAJI
Jumla ya viwanja 2161 vimepimwa katika eneo hilo la Nambogo na Katumba Azimio kwa matumizi mbalimbali ikiwemo makazi, makazi na biashara, shule, huduma za afya, maofisi, kituo cha biashara (Shopping Mall), vituo vya mafuta, viwanja vya michezo na maeneo ya kupumzikia.
viwango vya matumizi ya viwanja.
Na
|
Aina ya matumizi
|
Gharama kwa kila mita ya mraba
|
1
|
Makazi pekee (ujazo wa juu, kati na chini
|
2,700/= |
2
|
Makazi na biashara
|
3,000/= |
3
|
Biashara
|
5,000/= |
4
|
Huduma za jamii
|
3,500/= |
5
|
Ibada/ kuabudu
|
3,500/= |
6
|
Hoteli, vituo vya mafuta na maduka ya kuiwekezaji
|
5,000/= |
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani
Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA
Simu: 025 280 2137
Simu: 0739862632
barua pepe: ras@rukwa.go.tz
Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa