• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Utaratibu wa Kutoa Vibali vya Kusafirisha Mifugo ya kufuga au Biashara Kutoka Sehemu moja hadi Nyingine

Kumekuwa na wimbi la kusafirisha na kuhamisha mifugo ya kufuga bila kufuata taratibu kutoka eneo moja hadi jingine jambo ambalo linazua migogoro baina ya wakulima, wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi na kusababisha uharibifu wa mazingira na ueneaji wa magonjwa ya mifugo. Serikali ilikwishatoa Tamko la utaratibu wa kuhamisha mifugo ya kufuga kutoka sehemu moja hadi nyingine, mwaka 2006.

Vile vile Waraka wa Rais Na. 1 wa mwaka 2002 nao unakataza kabisa uswagaji holela wa mifugo katika maeneo yaliyo na barabara za lami, njia za reli au njia za maji na unawataka Wakuu wa Wilaya kulisimamia Agizo hilo.

Kwa kuzingatia maagizo ya Waraka wa Rais Na. 1 wa mwaka 2002, Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Na. 17 ya mwaka 2003 na Kanuni zake na Utaratibu kutoa vibali vya kusafirisha mifugo ya kufuga kutoka sehemu moja hadi nyingine ulitolewa ‘Taarifa kwa Umma’ mwaka 2006 na Katibu Mkuu wa iliyokuwa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo.

Mkoa unatoa maelekezo yafuatayo:-

1. Mifugo kwa ajili ya kufuga isihamishwe kutoka katika Kijiji ama Wilaya ama Mkoa kabla ya kupata Idhini/Kibali cha Kijiji, Wilaya ama Mkoa inakopelekwa.

Hivyo inapaswa Kijiji, Wilaya na Mkoa itoe kwanza idhini ya kupokea mifugo hiyo ya kufuga ndipo kibali cha kusafirisha mifugo (Animal Health Livestock Movement Permit) kitolewe kwa mujibu wa Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Na. 17 ya mwaka 2003 na Kanuni zake za mwaka 2007 (GN no.28), mwaka 2013 (GN no.225) na mwaka 2018 (GN no.475).

2. Kwa mujibu wa Utaratibu wa Serikali uliotolewa - Vijiji, Wilaya na Mikoa inapaswa isitoe Vibali vya kupokea mifugo ya kufuga kabla ya kujiridhisha kwamba wanayo maeneo ya kutosha ya malisho ya mifugo yaliyopimwa na kuthibitishwa na Wataalam kama yanafaa kwa malisho na yana maji ya kutosha.

3. Madaktari wa Mifugo wa Wilaya ndio wenye dhamana kisheria kutoa Vibali ‘Animal Health Livestock Movement Permit’ vya kusafirisha mifugo, na wanafanya hivyo kudhibiti ueneaji wa magonjwa ya mifugo nchini.

4. Kabla ya kutoa Vibali vya kusafirisha mifugo (Animal Health Livestock Movement Permit), Madaktari wa Mifugo wa Wilaya ama Wawakilishi wao waidhinishwa wahakikishe kwamba mifugo imeogeshwa na imechanjwa chanjo za kuzuia magonjwa husika kabla ya kuiruhusu mifugo hiyo kusafirishwa ili kuzuia uenezaji wa Magonjwa ya Mifugo.

5. Mifugo isafirishwe kwa njia isiyoharibu mazingira na miundombinu mingine kama ilivyoainishwa kwenye Waraka wa Rais Na. 1 wa mwaka 2002, Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Na. 17 ya mwaka 2003 na Kanuni zake.

(a) Kama mifugo inasafirishwa ndani ya maeneo ya Wilaya inapaswa kufuata njia rasmi za kupitisha mifugo zinazotambulika (Official stock-routes).

(b) Kama mifugo inasafirishwa kwenda nje ya Wilaya, Mkoa ama inatoka kwenye Minada ya Awali (Primary Livestock Markets) kwenda maeneo mengine ya ufugaji au Minada ya Upili/Mpakani (Secondary/Border Livestock Markets) inapaswa ipakiwe na kusafirishwa kwenye malori.

6. Ni jukumu la kila Halmashauri kuhakikisha kuwa inajenga na kutumia miundombinu ya kuwezesha mifugo kupakiwa na kushushwa kwenye magari pamoja njia rasmi za kupitisha mifugo zinazotambulika (Official stock-routes).

7. Usafirishaji wa Wanyama unapaswa kuzingatia pia matakwa ya Sheria ya Ustawi wa Wanyama Na.19 ya mwaka 2008 na Kanuni zake. Pamoja na Sheria nyingine za nchi, Kanuni na Miongozo mbalimbali iliyowekwa na Serikali.

Wilaya zinashauriwa zisimamie maelekezo haya kikamilifu na hatua za kinidhamu na kisheria zichukuliwe kwa Daktari/Mtaalamu wa Mifugo, Kiongozi wa Serikali ama Mfugaji yeyote atakayekiuka utaratibu huu.

Matangazo

  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAS Mchatta akagua miradi

    January 26, 2023
  • Wadau wa Elimu

    January 15, 2023
  • Ruwasa

    January 03, 2023
  • Waziri Mkuu Aanza Ziara Rukwa

    December 14, 2022
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa