• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Minerals

SEKTA YA MADINI

Umuhimu na nafasi ya sekta ya madini katika Mkoa.

Kama ilivyoelekezwa katika ibara ya 35 ya ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015- 2020 kuwa  serikali ya Mkoa  itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji  wanaohitaji kuwekeza katika madini.

Mkoa umesheheni rasilimali ya madini mbalimbali na vito. Hata hivyo, uchimbaji wa madini haya ni kwa kiasi kidogo na unaofanywa na wachimbaji wadogo. Mkoa unatambua umuhimu na nafasi ya madini katika kuchangia pato la taifa na la mwananchi mmoja mmoja. Kwa kulifahamu hilo, Mkoa unaweka mazingia mazuri ya upatikanaji wau meme, uboreshaji wa miundombinu ya barabara na mawasiliano ili kuvutia  wawekezaji kuja kuwekeza katika uchimbaji wa madini na vito ndani ya Mkoa.

Fursa za uwepo wa madini na vito zimetangazwa kwenye makongamano mbalimbali yaliyofanyika katika ndani na nje ya Mkoa (mwaka 2007 na Kanda ya Magharibi ya mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma miaka ya 2012, 2013 na 2014.) Aidha, maelezo hayo yanapatikana kwenye tuvuti ya Mkoa na Halmashauri.

Ofisi ya Madini Mkoa 

Katika mwaka wa fedha 2018/19, Tume ya Madini ilifungua Ofisi ya Madini Mkoa wa Rukwa (RMO – Rukwa). Ofisi hii imeanza kazi tarehe 09/11/2018 na inasimamia shughuli zote za madini katika Wilaya zote za Mkoa wa Rukwa na Halmashauri zake (Nkasi, Kalambo, Sumbawanga Manispaa na Sumbawanga Vijijini).

Soko la Madini

Ofisi ya Madini Mkoa wa Rukwa kwa kushirikiana Ofisi ya Katibu Tawala Mkoa tayari zimekwishaandaa miundombinu ya Soko la Madini. Tume ya Madini iko katika taratibu za kuliwezesha soko hilo kwa vifaa vya kitaalam ikiwamo mashine ya XRF na Geomological Tool Kit kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa kitaalam.

Pia kufuatia uchimbaji mwingi kuwa wa madini yasiyoweza kuuzwa sokoni mfano Mkaa wa Mawe na Madini Ujenzi, elimu imeendelea kutolewa kwa wachimbaji wenye leseni za uchimbaji wa madini yanayoweza kuuzwa sokoni kufanya uchimbaji endelevu utakaovutia wanunuzi wa madini kutoka maeneo mbalimbali nchini na nje ya nchi na maeneo ya mipakani Ofisi ya Madini imeendelee kushirikiana na vyombo vya Usalama kuweza kuwaelekeza watu wote kutoka nchi jirani kuingia na madini yao na kuyauza kwenye soko la madini.

Aina za madini yanayopatikana katika Mkoa wa Rukwa

Hadi kufikia tarehe 19 Februari, 2018 Mkoa ulikuwa na  jumla ya  watafiti 24 wenye leseni (Prospecting Licences) za kutafuta madini na wachimbaji wadogo 191 wenye leseni za uchimbaji wa madini (Primary Mining Licences) kwa vikundi au mmoja mmoja.

Aina za madini yanayopatikana katika Mkoa wa Rukwa

Na.

Madini

Yanakopatikana

Halmashauri

1
Copper 
Kasanga na Kapapa
Ifumwe
Kalambo
Nkasi
2
Zinc 
Kasanga na Kirando katika mwambao wa Ziwa Tanganyika
Kalambo na Nkasi.
3
Titanium and Zirconium 
Ntemba na Mkwamba
Nkasi
4
Emerald 
Mponda
Manispaa ya Sumbawanga
5
Aquamarine 
Mlombo kilometa chache mashariki mwa  bwawa la Kwela
Wilaya ya Sumbawanga
6
Burma Ruby 
Katuka, Chala na Kantawa
Wilaya Sumbawanga, Nkasi
7
Zircon 
Nzombo kijiji cha Matala.
Nkasi
8
Piezoelectric Quartz 
Kijiji cha Matala
Nkasi
9
Moonstone 
Mkombe Kaskazini mwa kijiji cha Kabwe mwambao wa ZiwaTanganyika
Nkasi
10
Green Tour- maline 
Chala, Swaila, Lyele na Tambaruka
Nkasi
11
Garnets 
Kantawa, Chala
Nkasi
12
Amethyst 
Kasu na Lyazumbi
Nkasi
13
Coal 
Muze, Namwele na Nkomolo
Wilaya ya Sumbawanga na Nkasi
Manispaa ya Sumbawanga
14
Kaolin 
Kufuata Barabara ya Sumbawanga  hadi Kasanga
Sumbawanga na Kalambo
15
Limonite 
Mbuga/ Namwele
Manispaa ya Sumbawanga
17
Kyanite
Kizi, Chala na Tambaluka
Nkasi
18
Helium gas
Bonde la Ziwa Rukwa

Chanzo: Ofisi ya madini ya Kanda (Mpanda) 

Kwa mujibu wa takwimu kutoka Ofisi ya Madini Kanda yetu ya Magharibi, madini yanayochimbwa zaidi katika mkoa wa Rukwa ni makaa ya mawe na Madini ya ujenzi. Kiasi cha makaa ya mawe yaliyochimbwa mwaka 2007–2008 eneo la Namwele lililopo Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ni tani  3,692.7 yenye thamani ya Shilingi 107, 669,167. Makaa hayo yaliyochimbwa na Kampuni ya Upendo Group Limited yaliuzwa kwenye kiwanda cha Mbeya Cement.

 


 Uwepo wa gesi ya Helium katika Mkoa

Taarifa ya tarehe 19 Februari, 2018 kutoka Ofisi ya Madini ya Kanda-Mpanda inaeleza kuwa mwezi Mei, 2016 Kampuni ya Helium One Ltd. inayomiliki leseni 8 za utafutaji wa Gesi ya Helium Mkoani Rukwa kupitia Kampuni zake tanzu za Togota (T) Limited, Njozi (T) Limited na Stahamili (T) Limited iligundua uwepo wa Gesi ya Helium Mkoani Rukwa. Kwa mujibu wa makadirio yaliyofanyika, inaonesha kwamba Gesi hii ipo kwa kiasi kisichopungua futi za ujazo Bilioni hamsini na nne (54cf).

Kampuni inatarajia kuanza kufanya uchorongaji kabla ya mwezi Julai mwaka huu (2018) kwa lengo la kupata kiasi halisi kilichopo katika eneo hilo ili uchimbaji uanze rasmi. Maeneo ilipogundulika Gesi hii ni Kusini Mashariki mwa Ziwa Rukwa eneo la Gua na Mto Lwiche kwa upande wa Magharibi mwa Ziwa Rukwa. Upatikanaji huu wa Gesi ya Helium utachangia kwa kiasi kikubwa maendeleo ya Mkoa wa Rukwa na Nchi kwa ujumla.

Ombi kwa Wawekezaji

Kutokana na fursa hizo za madini mbalimbali kuwepo katika Mkoa hii inamaanisha uhitaji wa huduma mbalimbali kwa watumishi wa migodi hii kama vile shule, vyakula, hoteli za kisasa, kumbi za mikutano, n.k 

Matangazo

  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RAS Mchatta akagua miradi

    January 26, 2023
  • Wadau wa Elimu

    January 15, 2023
  • Ruwasa

    January 03, 2023
  • Waziri Mkuu Aanza Ziara Rukwa

    December 14, 2022
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa