• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Abiria wanaotoka mikoa iliyoathirika kukaa Karantini Rukwa huku wananchi wakitakiwa kuvaa barakoa.

imewekwa Tar: April 21st, 2020

Katika harakati za kupambana na ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (COVID – 19) Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa maelekezo kwa wananchi wa mkoa wa Rukwa kuhakikisha wanavaa barakoa wanapokuwa katika mikusanyiko pamoja na maeneo yao ya kibiashara hasa kwa wale wanaohusika na kutoa huduma kwa jamii huku akivitaka vyombo husika kuhakikisha abiria wote wanaotoka katika maeneo yaliyoathirika ndani ya nchi kuingia mkoa wa Rukwa washauriwe kujitenga kwa hiari kwa muda wa siku 14.

Mh. Wangabo amesema kuwa abiria hao wanaoingia ndani ya mkoa wanatakiwa kupimwa afya zao kwa kipima joto (Thermal Scanner) kwenye vituo vitatu vya mabasi mkoani humo ikiwemo Laela kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, Kituo cha mabasi Namanyere kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi pamoja na kituo kikuu cha mabasi Sumbawanga na kuongeza kuwa abiria hao wanatakiwa kuvaa Barakoa.

“Abiria wanaoingia Mkoa wa Rukwa kutoka kwenye maeneo yaliyoathirika wanashauriwa kujitenga wao wenyewe kwa hiari yao kwa muda wa siku kumi na nne (14). Endapo watahisi au kugundua kuwa wanaona dalili zozote za matatizoya kiafya watatakiwa kuripoti kwenye kituo chochote cha Afya cha karibu,” Alisema.

Aidha, Mh. Wangabo amewashauri wafanyabiashara wote ndani ya mkoa wenye tabia za kusafiri kwa nia ya kufuata mizigo ya kibiashara kuacha kufanya hivyo na badala yake wajenge tabia ya kuagiza bidhaa hizo kwa njia ya sim una kulipa kwa njia za mitandao ya simu ama benki inapobidi na pia kuwashauri wafanyabiashara wadogo kujiunga na kuagiza mzigo kwa pamoja ili kuwa na urahisi wa kupata usafiri wa pamoja.

“Watu wote wanaofanya kazi za kutoa huduma kwenye maduka, Maeneo yote ya kuuza vyakula, Saluni, Super Market, Wahudumu wa nyumba za kulala Wageni wanatakiwa kuvaa barakoa. Familia zinapotaka kufanya manunuzi ya jumla, inashauriwa aende mtu mmoja tu kutoka kila familia kufanya manunuzi hayo. Hata kwenda hospitali kuona wagonjwa aende mtu mmoja tu na mtu huyo asisahau kuvaa barakoa,” Alisisitiza.

Halikadhalika, amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa minada yote na Magulio inadhibitiwa na kuendeshwa kulingana na maelekezo ya wataalamu wa afya na serikali kwa ujumla, na kubainisha kuwa serikali ya mkoa haitasita kusitisha mnada ama gulio endapo taratibu na maelekezo ya wataalamu ama ya serikali yatakiukwa.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika taarifa yake aliyoitoa leo tarehe 20.4.2020 kwa vyombo vya habari.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu hadi kufikia tarehe 20.4.2020 watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Corona nchini ni 254 ambapo kati ya hao mkoa wa Rukwa ina wagonjwa wawili (2)

Matangazo

  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Kodi kwa Maendeleo September 15, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chanjo Polio

    May 18, 2022
  • NFRA

    May 11, 2022
  • Vyama vya Ushirika

    May 05, 2022
  • Eng. Kundo: Nimeridhishwa na Zoezi la Anwani za Makazi Rukwa

    April 27, 2022
  • Angalia Zote

Video

RC Mkirikiti akabidhiwa Ofisi Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0764902066

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa