• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

“Enzi ya kufunga Sukari kwenye gazeti kurudi tena” RC Wangabo

imewekwa Tar: June 2nd, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatahadharisha wananchi wote watakaotumia mifuko ya plastiki kwa kuitumia kiuza, kusambaza, kubebea ama kuimiliki kwa namna yoyote ile kwani kwa kufanya hivyo watahatarisha uhuru wao na kuongeza kuwa kutokana na gharama kuongezeka ili kuipata mifuko mbadala amewataka wananchi kuanza kutumia mifuko ya kaki ama magazeti ya zamani kufungia sukari ama unga.

Amesema kuwa Mkoa umejipanga na wataalamu wake mbalimbali watendaji, kuanzia ngazi ya vitongovi, vijiji, mitaa, kata, halmashauri na wilaya zote kuhakikisha mifuko hiyo ya plastiki haitumiki na kubainisha kuwa kwasababu kanuni zipo na zimefafanua vizuri hivyo hakuna sababu za kutafuta visingizio ili kuweza kukwepa adahabu kwa atakayekiuka sheria hiyo.

“Tutaendelea kuona ni changamoto gani ambazo zinatukabili sisi, najua kama nilivyosema mifuko mbadala huenda isiwe mingi sana lakini hii haizuii watu kufanya shughuli zao kubebea, kuna vitu vingi, kuna vikapu, mbona zamani tulikuwa tunatumia mifuko ile ambayo ni ya kaki, unatengeneza unaweka gundi, lakini ukienda kwenye duka unakuta zile karatasi za magazeti wanakukunjia wanakuwekea sukari yako mule unaondoka, tutarudi huko,” Alisisitiza

Na kuongeza kuwa kadiri siku zinavyozidi kusogea mifuko mbadala itajaa na pia alitumia fursa hiyo kuwaasa wajasiliamali kuitumia fursa kuweka viwanda vidogovidogo vya kuzalisha mifuko mbadala.

Katazo hilo limetokana na Sheria ya Usimamizi wa Mazingira (Environmental Management Act) serikali ya Tanzania imetunga kanuni za mwaka 2019 za kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki.

Kifungu cha nane cha kanuni hizo kinaorodhesha makosa matano ambayo ni; kuzalisha na kuagiza mifuko ya plastiki, kusafirisha nje ya nchi mifuko ya plastiki, kuhifadhi na kusambaza mifuko ya plastiki, kuuza mifuko ya plastiki na mwisho kumiliki na kutumia mifuko ya plastiki.

Kila kosa lina adhabu yake kwa mujibu wa kanuni hizo kulingana na uzito wa kosa lenyewe.

Kwa kosa la kwanza la uzalishaji na uagizaji adhabu yake ni mosi,faini isiyopungua TSh milioni 5 na isiyozidi TSh milioni 20, pili kifungo kisichozidi miaka miwili jela, adhabu ya tatu ni mjumuiko wa adhabu zote mbili za awali faini na kifungo.

Adhabu za kosa la pili amabalo ni kusafirisha mifuko nje ya Tanzania ni sawa na za kosa la kwanza.

Kwa kosa la tatu la kuhifadhi na kusambaza mifuko adhabu zake ni mosi faini isiyopungua TSh milioni 5 na isiyozidi TSh miioni 52, pili kifungo kisichozidi miaka miwili, tatu faini na kifungo kwa pamoja.

Ukipatikana na hatia ya kuuza mifuko ya plastiki adhabu ambazo utakumbana nazo ni mosi, faini isiyopungua TSh laki moja na isiyozidi laki tano, pili, kifungo kisichozidi miezi mitatu jela na tatu yawezekana ukahukumiwa adhabu zote mbili za awali kifungo na faini.

Ukiendelea kutumia na kumiliki mifuko ya plastiki kuanzia Juni 1 nchini Tanzania, basi jiandae kulipa faini isiyopungua TSh30,000 na isiyozidi laki mbili, kifungo kisichozidi siku saba ama faini na kifungo.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa