• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kamatiya Amani Rukwa waipongeza NEC huku RC akionya watakaoleta vurugu

imewekwa Tar: November 1st, 2020

Viongozi wa Kamati ya Amani Mkoani Rukwa Wameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa utaratibu mzuri waliouweka katika vituo vya kupigia kura hali iliyopelekea kuondoa msongamano na wapiga kura kutimiza haki yao ya kikatiba bila ya bugudha wala kupoteza muda kwa kusimama kwenye foleni muda mrefu katika vituo hivyo.

Aidha, viongozi hao wametanguliza Shukrani zao kwa Mwenyezi  Mungu kwa kujalia hali ya utulivu na amani wakati wote wa kupiga kura na kuwashukuru Watanzania kwa kuzingatia maelekezo ya Tume katika muda wote wa zoezi hilo.

Akizungumza kwa niaba ya kamati hiyo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Askofu Ambele Mwaipopo wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Ziwa Tanganyika alisema, “Tumeshuhudia katika vituo vyetu vya kupigia kura hali ikiwa shwari kabisa, na wapiga kura katika maeneo mengi nchini wameshuhudia kuwa kulikuwa na utengamano na utulivu mkubwa san ana tunawashukuru watanzania kwa kuzingatia maelekezo ya Tume mathalan, mara baada ya kupiga kura rudi nyumbani ili kupisha msongamano na karibu wote walifanya hivyo.”

Halikadhalika, Askofu Mwaipopo amewaomba watanzania kuendeleza utulivu wakati huu ambapo matokeo ya kura katika majimbo bado yanaendelea kutangazwa hadi pale wateule kwa nafasi ya Rais, Wabunge na Madiwani watakapokula nyapo zao.

“kikubwa ni kwamba baada ya haya matokeo kutangazwa, tuvunje makambi yetu ya kisiasa na kutoa ushirikiano kwa wale wote walioshinda na ikumbukwe kwamba, kwa nafasi ya Urais, iwe ama ulimchagua au la, ni Rais wako, vivyo hivyo kwa Wabunge na Madiwani, Ni uungwana na Uzalendo kwa Taifa letu kushikamana na kuwa wamoja kwaajili ya maslahi mapana ya nchi yetu,” Alisisitiza.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaasa waanchi wa mkoa wa Rukwa kuendeleza utulivu akiamini kuwa wanarukwa hawawezi kudanganywa na watu ambao wanadhamira ya kuanzisha vurugu baada ya kushindwa na kuwasihi kujikita kwenye masuala ya kilimo baada ya kumaliza zoezi la kuwachagua viongozi wawapendao.

“Kuna watu ambao kula yao ipo huko, akichochea ndio anaenda kula lakini wewe usipokwenda kulima hutakula, kwahiyo wanachi wawapuuze, hasa vijana, wawapuuze watu wote ambao wanataka kutuletea vurugu, lakini pili niwaonye wale wote wanaotaka kujaribu kutuvuruga ndani ya Rukwa wasijaribu, vyombo vya ulinzi na usalama viko macho sana, tuko vizuri mno tumejipanga, yeyote atakayeleta vurugu tutamshughulikia ipasavyo, tena kwa ukamilifu,” Alisisitiza.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO POLIO

    September 15, 2023
  • HALI YA USALAMA KABWE NI SHWARI, KAZI IENDELEE

    September 12, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa