• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

“Kwa gharama yoyote ile michezo lazima ikue Rukwa” RAS Rukwa.

imewekwa Tar: October 10th, 2017

Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bernard Makali ameahidi kusimamia michezo katika Mkoa wa Rukwa na kuhakikisha Mkoa haubaki nyuma katika mashindano mbalimbali ya kitaifa ikiwemo ligi kuu ya soka Tanzania bara

Bernard Makali ambaye pia ni Mwenhyekiti wa baraza la Michezo la Mkoa amesema kuwa michezo yote itasimamiwa kuanzia ngazi ya mtaa, kata na wilaya na kuwashirikisha wadau wote kuanzia mwananchi wa kawaida, madiwani, wabunge na taasisi za kiserikali na zisizo za kiserikali zilizopo katika mkoa ili kusukuma maendeleo ya michezo katika Mkoa.

“Michezo yote itasimamiwa, siyo mpira peke yake, lazima wadau wote washirikishwe katika mkoa ili kukuza michezo katika mkoa wetu, kuna mama hapa amelalamika wanawake hawachezi, lakini kuna chama cha netiboli tumekiwezesha kwenda Dodoma kwenye uchaguzi wao na wamefanikiwa, hivyo wote wanawake kwa wanaume watashiriki kwenye michezo,” Makali alisisitiza

Aliyaongea maneno hayo alipoitisha kikao cha wadau wa michezo wa mkoa kabla ya kukabidhi mipira 100 iliyotolewa na chama cha mpira wa miguu taifa (TFF) kwa vilabu 20 vya watoto vilivyopo katika Mkoa wa Rukwa.

Pia aliviagiza vilabu vyote na viongozi wa vyama mbalimbali vya michezo waliohudhuria kikao hicho kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kutekeleza agizo la Makamu wa Rais wa Nchi mama Samia Suluhu la kufanya mazoezi kila jumamosi ya pili ya mwezi ili kuhamasisha michezo pamoja na kuimarisha afya za wanarukwa.

“Mkoa huu hatuhamasishi wananchi kufanya mazoezi katika jumamosi ya pili ya mwezi, sasa naagiza sisi tuliopo ndani hapa tuwahamasishe wananchi huko tunapoishi kufanya mazoezi, na nataka kuona ratiba ya kila kilabu kujua wanapofanyia mazoezi kila siku hna hasa jumamosi ya pili ya mwezi,” Alimalizia.

Katika kikao hicho wadau hao walielezea changamoto mbali mbali za michezo mkoani Rukwa ikiwemo kutokuwa na ushirikiano kati ya chama cah mpira cha Mkoa pamoja na vyama vya mpira vya Wilaya jambo linalopelekea kudhoofisha maendeleo ya mpira katika mkoa.

Akizungumzia migogoro iliyopo katika vyama hivyo na namna wanavyoendelea kuitafutia ufumbuzi Mwenyekiti wa Chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Rukwa (RUREFA) Bw. Blas Kiondo amesema kuwa tangu aingie madarakani mwaka 2013 amekuwa akikabiliana na changamoto hiyo na kuahidi kuimaliza kabisa.

Kwa upande wake Afisa michezo wa Mkoa Gabrieli Hokororo ametahadharisha kuwa si vyema kuyafufua makovu na badala yake wadau waungane pamoja ili kupeleka maendeleo ya michezo mbele na hatimae Mkoa wa Rukwa usikike kwenye ramani ya michezo katika taifa.

Matangazo

  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAWEKEZAJI KUTOKA ZAMBIA WAVUTIWA NA BANDARI MKOANI RUKWA

    May 28, 2023
  • MRADI WA MAJI WAZINDULIWA KISA

    May 15, 2023
  • ZAHANATI YA MPONA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA YAZINDULIWA

    May 15, 2023
  • UPENDO, MAADILI NA FAMILIA IMARA MUAROBAINI WA UKATILI WA KIJINSIA

    May 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa