• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Mikataba Lishe

imewekwa Tar: October 19th, 2022

USTAWI WA FAMILIA UNATEGEMEA LISHE BORA- RC SENDIGA

Na. OMM Rukwa

Halmashauri za mkoa wa Rukwa zimesema zitaendelea kuhakikisha zinatenga na kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji afua za lishe ili kukabiliana na tatizo la udumavu na utapiamlo kuathiri afya ya watoto chini ya miaka mitano

Akizungumza kwa niaba ya madiwani wa mkoa wa Rukwa, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Justin Malisawa alisema wakiwa wasimamizi wakuu wa halmashauri watahakikisha kila robo mwaka fedha za afua za lishe zinatengwa na kutolewa kwa jamii.

Malisawa amesema hayo leo (Oktoba 19, 2022) mjini Sumbawanga wakati wa hafla ya utiaji saini mikataba ya utekelezaji afua za lishe kati ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga na Wakuu wa Wilaya za Sumbawanga, Nkasi na Kalambo.

“Sisi madiwani tutaendelea kuhakikisha kila matumizi ya halmashauri ya miezi mitatu fedha za lishe zinatengwa na kupelekwa katika utekelezaji wa agenda za lishe .Suala la lishe endelevu litaendelea kupewa kipaumbele”alisema Malisawa.

Akifungua kikao hicho, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga aliwataka wakuu wa wilaya kuhakikisha mikataba waliyosaini inakwenda kutekelezwa hadi ngazi ya chini kwa watendaji kabla ya ifikapo Oktoba 25 mwaka huu.

Sendiga alibainisha kuwa mkataba huo ni maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kunakuwa na utekelezaji wa afua mbalimbali za lishe katika jamii ili kupunguza kiwango cha udumavu ambacho mkoa wa Rukwa ni asilimia 47.9.

“Maelekezo yangu kwa Wakuu wa Wilaya, mkasimamie wilaya zenu kuhakikisha fedha zilizopangwa kutekeleza afua za lishe zinatolewa kwa wakati. Aidha, taasisi zote zinazoshughulikia suala la lishe katika mkoa zijulikane ili iwe rahisi kufuatilia mipango yao utekelezaji “alisisitiza Sendiga.

Naye Mratibu wa Mradi wa Lishe Endelevu mkoa wa Rukwa Maria Machilu alisema suala la vikao vya kamati za lishe lipewe kipaumbele kwenye halmashauri ili kuwezesha jamii kushiriki kupanga mikakati ya kupunguza udumavu ikiwemo elimu ya lishe bora.

Mkoa wa Rukwa katika tathmini ya lishe iliyofanyika jijini Dodoma Septemba 30 mwaka huu ilitangazwa kushika nafasi ya kwanza kitaifa kwa utekelezaji mzuri wa afua za lishe.

Mwisho

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO POLIO

    September 15, 2023
  • HALI YA USALAMA KABWE NI SHWARI, KAZI IENDELEE

    September 12, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa