• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Rukwa aishauri benki ya NMB kufungua tawi bonde la ziwa Rukwa.

imewekwa Tar: October 3rd, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen ameishauri benki ya NMB kufungua tawi katika bonde la Ziwa Rukwa ili kusogeza huduma hiyo karibu na wananchi ambao shughuli zao kubwa za kiuchumi ni kilimo cha mahindi, mpunga pamoja na uvuvi.

Amesema kuwa kwa kufanya hivyo kutaepusha matukio ya uvamizi na mauaji yanayofanywa na baadhi ya watu wanaowavizia wakulima na wafanyabiashara wanaoweka fedha majumbani mara tu baada ya mauzo ya mazao yao.

“Mimi nashauri Benki ya NMB muwe na Tawi huku, si lazima kuwa na jengo, hata ile Mobile Banking ambayo mwananchi anaweza kupata huduma zote za kuweka na kutoa fedha katika gari hiyo, ili fedha zao hawa ziwe katika mikono salama,” Mh. Zelote Alisema.

Ametoa ushauri huo katika ufunguzi wa siku ya huduma kwa wateja iliyofanywa na benki ya NMB kanda ya nyanda za juu katika Kijiji cha Mfinga, kata ya Mfinga, Wilaya ya Sumbawanga, kabla ya kukabidhi vifaa vya shule pamoja na hospitali vyenye thamani ya Shilingi milioni 20.

Sambamba na hilo Mh.Zelote amewahamasisha wakulima pamoja na wafanyabiashara wa Kata ya Mfinga kufungua akaunti benki na pia kujiunga katika vikundi ili kuwa na urahisi wa kupata mikopo  na kuweza kuwainua kiuchumi.

“Mbali na kuhifadhi fedha pia benki inatoa mikopo kwaajili ya kujiendeleza na hatimae kuwainua wakulima waweze kuongeza thamani ya mazao yao na kupata soko pana hasa katika awamu hii inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli inayohamasisha uchumi wa viwanda kwa taifa,” Alisema.

Aidha aliwataka viongozi wa Kijiji na wanufaika wa vifaa hivyo kuvitumia vifaa hivyo kwa malengo yaliyokusudiwa na ikiwemo kuwahudumia wananchi bila ya bugudha na kuonya kuwa wananchi wasiogope kuwashitaki watumishi wanaowahudumia kwa viburi.

Awali akisoma taarifa fupi ya Benki ya NMB Mkurugenzi wa Huduma kwa wateja makao makuu ya benki hiyo Richard Makungwa alisema kuwa Benki ya NMB hutenga asilimia moja ya mapato kwa mwaka ili kuirudishia jamii na kuweza kuisaidia katika mambo mbalimbali ikiwemo elimu na afya.

“Kwa kuunga mkono juhudi za Rais wetu tumeamua kama Benki kutoa kompyuta 7, vitanda 8 vya kulalia, vitanda 4 vya kujifungulia, magodoro 8 pamoja na mabati 204 vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 20 vilivyotolewa na benki hiyo kama marejesho ya faida kwa wateja watu,” Alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji hicho Godfrey Kalungwizi aliahidi kuvisimamia vifaa hivyo na kuendelea kuwahamasisha wananchi kuchangia katika shughuli za kimaendeleo.

Matangazo

  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAWEKEZAJI KUTOKA ZAMBIA WAVUTIWA NA BANDARI MKOANI RUKWA

    May 28, 2023
  • MRADI WA MAJI WAZINDULIWA KISA

    May 15, 2023
  • ZAHANATI YA MPONA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA YAZINDULIWA

    May 15, 2023
  • UPENDO, MAADILI NA FAMILIA IMARA MUAROBAINI WA UKATILI WA KIJINSIA

    May 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa