• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Rukwa awataka wananchi kujiandaa kuandikishwa vitambulisho vya uraia.

imewekwa Tar: April 13th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amewataka wananchi kuwa na viambatanisho vya muhimu vitakavyowatambulisha kwa urahisi katika zoezi la uandikishwaji wa vitambulisho vya uraia.

Mh. Zelote ametoa rai hiyo alipokuwa akizindua na kukabidhi vitambulisho kwa baadhi ya watumishi wa Mkoa, Wilaya pamoja na Halmashauri.

“Andaeni viambatanisho muhimu vitakavyowasaidia kutambulika kwa urahisi.Viambatanisho vya msingi ni pamoja na vile vinavyohitajika kuthibitisha umri, Makazi na Uraia, kama vile cheti cha kuzaliwa, hati ya kusafiria, Vyeti vya shule, kadi ya kupigia kura, kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, TIN namba n.k. Kuwa na vitambulisho vingi ni kutambulika kwa haraka na kurahisisha uandikishaji,” Mh. Zelote alifafanua.

Zoezi hili la vitambulisho vya taifa lilianza kwa watumishi wa umma tarehe 3, October hadi 31, Disemba mwaka 2016, na kutegemewa kuanza uandikishwaji huo mnamo mwezi wa 6 mwaka huu kwa wananchi wote wa Mkoa wa Rukwa.

Mkuu wa Mkoa pia hakusita kutoa ushauri kwa watendaji wa Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa kuhakikisha wanaweka utaratibu mzuri ili kuwawezesha kila mwananchi kujiandikisha bila ya usumbufu.

Pamoja na hayo Mh. Zelote aliwatahadharisha kuwa katika uandikishwaji huo watakutana na watu aina tofauti hivyo ni jukumu lao kupanga namna ya kurahisisha huduma hiyo.

“Mkumbuke mtakutana na watu wa aina tofauti wakiwepo wazee,  vijana, walemavu na  waja wazito.  Ni jukumu lenu kujipanga namna ya kurahisisha huduma kwao.  Toeni ratiba zenu mapema kuwandaa wananchi.  Shirikianeni na Watendaji wa Halmashauri ngazi ya Vijiji, Kata n.k.” Mh Zelote alieleza.

Katika kusisitiza suala la ushirikiano Mh. Zelote aliwaomba viongozi wa dini na siasa kutoa ushirikiano kwa kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na kwa wakati na kujitokeza katika zoezi hili.

Miongoni mwa faida za vitambulisho hivi ni pamoja na kusaidia kuongeza wigo wa mapato ya serikali, kurahisisha kuhesabu watu, vitawezesha kumtambua mtu anapofanya biashara au shughuli nyingine kwa kutumia majina tofauti n.k.

Nae Afisa NIDA Mkoa wa Rukwa Emmanuel Mujuni aliwaomba wananchi kuwa na subira hadi hapo utaratibu utakapokamilika na kuweza kuwatangazia na hatimae zoezi hilo kuanza mara moja.

Matangazo

  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Kodi kwa Maendeleo September 15, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC Sendiga: Tutafanya Mapinduzi ya Kilimo Rukwa

    August 11, 2022
  • RC Sendiga: Niko Tayari kwa Kazi

    August 09, 2022
  • Sensa

    July 10, 2022
  • Maandalizi ya Sensa Rukwa

    July 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

RC Mkirikiti akabidhiwa Ofisi Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0764902066

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa