• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo aiagiza SUWASA kuwakatia maji wenye madeni sugu.

imewekwa Tar: December 3rd, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh.Joachim Wangabo ameiagiza Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Sumbawanga (SUWASA) kuwakatia maji wateja wenye madeni sugu ili waweze kulipa madeni yao wanayodaiwa na taasisi mbalimbali za serikali nchini.

Amesema kuwa uendeshaji wa Mamlaka hiyo utaendelea kuwa mgumu endapo wataendelea kuwafumbia macho wateja wanaowadai na kushauri kuanza kuangalia namna ya kutumia kadi za “pre- paid” (malipo ya kabla) katika huduma hiyo ya maji ili kuzuia madeni yatokanayo na malipo baada ya matumizi.

“lazima muwabane walipe madeni, ni kama umeme kama mtu halipi Kata, na huku kata maji, kama umewekwa utaratibu basi uheshiumiwe huo utaratibu, nimesikia kwenye taafifa hapo kwamba kuna upungufu wa fedha makudsanyo madogo na matumizi makubwa na wakati huo huo mna madeni makubwa na watu hawalipi, kata,” Mh. Wangabo alisisitiza.

Ametoa kauli hiyo alipofanya ziara yake ya kwanza kwa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Sumbawanga (SUWASA) ili kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na mamlaka hiyo pamoja na kuufahamu kwa kina mradi wa Maji safi na usafi wa mazingira katika miji saba nchini Sumbawanga ikiwemo, chini ya MDG – Initiative unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya pamoja na Serikali ya Ujerumani wenye thamani ya Bilioni 31.

Aidha ameendelea kuwasisitiza Mamlaka hiyo kwa kushirikiana na Manispaa pamoja na vyombo vya usalama kuhakikisha vyanzo vya maji vinahifadhiwa na kupiga marufuku wale wote wanaofanya shughuli za kibinaadamu katika vyanzo vya maji na kuwachukulia hatua wale wanaokiuka sheria hiyo ya mazingira.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa SUWASA Hamis Makala amesema Mamlaka hiyo inadai taasisi za kiserikali Shilingi Milion 69 na pia inadai watu binafsi shilingi milioni 250 huku Mamlaka hiyo ikiwa inadaiwa shilingi milioni 100.6, na kuongeza kuwa miongoni mwa changamoto wanazozipata ni kukauka kwa vyanzo vya maji.

“Hadi Novemba mwaka 2017, SUWASA inadaiwa Milioni 100.6 kutoka kwa wadaiwa wake, mgawanyo wa madeni ni; Madawa ya Maji Shilingi Milioni 14.5, TRA Shilingi Milioni 13, EWURA Shilingi Milioni 6.8, Fidia Shilingi Milioni 32, TANESCO Shilingi Milioni 17, Mita za Maji Shilingi milioni 6, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Shilingi Milioni 11 kwaajili ya hati miliki,” Makala alifafanua.

Halikadhalika Makala alisema kuwa deni hilo limekuwa kubwa zaidi baada ya mkandarasi Herkin Builders kudai Shilingi Milioni 247.6 kama riba ya kucheleweshewa malipo ya kujenga mradi wa dharura wa maji safi Sumbawanga kati ya mwaka 2009 hadi March 2016.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa