• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

imewekwa Tar: April 5th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatoa wasiwasi wananchi Mkoani Rukwa ambao bado wamekuwa wakijiuliza maswali juu ya uelekeo wa serikali na nchi baada ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kilichotokea tarehe 17.3.2021.

Mh. Wangabo amesema kuwa tangu nchi hii ipate uhuru mwaka 1961 ni miaka 60 imepita na sasa imepata rais wa Sita Mwanamke, tukio ambalo ni la kihistoria na kuongeza kuwa kinamama kwa miaka mingi wamekuwa shupavu katika kuongoza familia hasa malezi ya Watoto na hivyo kuwaomba wananchi wote kuziongoza familia zao kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan ilia pate nguvu na Afya na kuleta maendeleo katika nchi yetu.

“Najua kila mmoja wetu sasa hivi anatafakari kwa kina kwamba nchi sasa hivi tunaelekea wapi, niwahakikishie kwamba serikali ipo, inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo na sisi tupo, tunachotaka sisi ni amani ili nchi iweze kusonga mbele, lakini kikubwa Zaidi niwaombe tuendelee kumuombea Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia, tumuombee san ana tuwaombee viongozi wote wa serikali ili serikali yetu isiyumbe iwe thabiti na kwa maongozi ya Mwenyezi mungu tutafika.”

“Sina shaka, Rais wetu anatutosha, lakini anahitaji kuungwa mkono, mshikamano na amani na utulivu kutoka kwetu, bila ya shaka wanarukwa wote, tunalifanya hili na tumeanza kulifanya na tutaendelea kulifanya la kuleta amani, na tumeshuhudia tuna amani ya kutosha, tuendelee nayo, lakini tusione mtu ana ngeu ama amevunjika mguu kesho ama keshokutwa, mtaleta dosari,” Alisisitiza.

Mh. Wangabo ameyasema hayo alipokuwa akitoa salamu zake za Pasaka katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Mjini Sumbawanga baada ya Ibada ya Pasaka ambapo wakristo wote nchini wanaungana na wenzao duniani kusheherekea sikukuu hiyo.

Aidha, katika kuhakikisha Watoto yatima hawaachwi nyuma Mh. Wangabo alipitisha ‘Bakuli’ kwa waumini waliohudhuria ibada hiyo ili kupata fedha za kununua baadhi ya mahitaji kwaajili ya Watoto yatima wa kituo cha Mtakatifu Maria Goreth kilichopo Katandala mjini Sumbawanga, ambapo katika mchango huo ilipatikana Shilingi 188,600/= na kuzikabidhi kwa Padri Canute Mwageni Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme Mjini Sumbawanga

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa