• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Udhibiti wa Kipindupindu

imewekwa Tar: September 28th, 2022

SERIKALI KUDHIBITI UGONJWA WA KIPINDUPINDU - DKT.MNKENI

Na. OMM Rukwa

Afisa Mpango wa Taifa wa Afya Shuleni toka Wizara ya Afya Dkt. Emmanuel Mnkeni amesema serikali itaendelea kuchukua hatua kudhibiti mlipuko wa magonjwa ikiwemo kipindupindu.

Dkt. Mnkeni alisema mafunzo kwa Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii ( CHWs), Walimu na Wenyeviti wa kamati za Shule yanalenga kuhamasisha jamii kuhusu ujenzi wa vyoo bora na usafi wa mazingira ili kudhubiti magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.

Mafunzo hayo yametolewa leo ( 27.09.2022) katika kijiji cha Kirando Wilaya ya Nkasi ambapo Wizara ya Afya inalenga kuhamasisha na kuelimisha viongozi na jamii kushirikiana ili kuweka utamaduni wa kutumia vyoo bora.

" Wizara ya Afya kwa kushirikana na OR- TAMISEMI inaendelea kutoa elimu endelevu ili jamii iweze kubadilika kwa kutumia vyoo bora,kunawa mikono kwa maji tiririka pamoja na kunywa maji safi na salama" alisema Dkt. Mnkeni.

Kwa upande wake Peter Muna ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi Mkinga alisema Sheria ndogo ziendelee kutumika hata pale ugonjwa wa kipindupindu unapoisha na kuwa viongozi wa vijiji wawe mfano wa kuigwa kwa kuwa na vyoo safi na kuvitumia.

Naye Mwalimu Betty Sungura toka Shule ya Msingi Mpata kata ya Kirando aliiomba serikali iongeze nguvu katika upatikanaji wa miundombinu ya kutosha ya matundu ya vyoo ili watoto waepuke mlundikano wanapoenda chooni.

" Miundombinu mibovu ya vyoo kinakuwa chanjo cha mlipuko wa magonjwa hususan pale shule inapokuwa na msongamano wa watoto" alisema Mwalimu Sungura.

Kwa upande wake Afisa Elimu ya Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Augustine Bayo alibainisha kuwa viongozi wa vijiji na kata ndio wenye jukumu la kuhakikisha wanafunzi wakuwa na vyoo bora na vinatumika .

Bayo aliongeza kusema serikali inajitahidi kutenga fedha za kuwezesha ujenzi wa miundombinu ya vyoo kupitia mradi wa SWASH.

"Kila kaya au shule lazima iwe na vyoo bora ili kudhibiti mlipuko wa magonjwa ikiwemo kipindupindu " alisema Bayo.

Wilaya za Nkasi na Kalambo kwa nyakati tofauti zimekuwa na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.

Kipindupindu ni ugonjwa wa kuharisha na kutapika unaosababishwa na vimelea vya bakteria vinavyoitwa kwa lugha ya kitaalam " Vibrio cholera" na madhara yake ni pamoja na vifo.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO POLIO

    September 15, 2023
  • HALI YA USALAMA KABWE NI SHWARI, KAZI IENDELEE

    September 12, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa