• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Uvivu wa Vijana wa Kiume Mkoani Rukwa wamkasirisha RC Wangabo

imewekwa Tar: June 11th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa mh. Joachim Wangabo amesikitishwa na uvivu wa kutofanya kazi kwa vijana wa kiume katika mkoa hali inayopelekea miradi mingi inayotekelezwa na serikali katika mkoa huo kwa kutumia force account inafanywa na vijana wanaotoka nje ya mkoa huo jambo ambalo sio madhumuni ya serikali ya awamu tano.

Amesema kuwa lengo la ujenzi kwa kutumia force account ni kuhakikisha kwamba wananchi wa maeneo husika wanapata manufaa ya ujenzi ule na kufanya ujenzi huo kuwa ni wa kwao na kujivunia kwamba walishiriki tangu mwanzo wa ujenzi huo kuanzia ngazi ya songambele ya kuchimba msingi hadi kumalizika kwa majengo hayo

“Watu wameshiriki kweny songambele hapa lakini baadae tunapotafuta vibarua wa kufanya kazi, mtu anafanya siku mbili, siku tatu akipewa malipo yake anapotea, Uvivu, sasa hii tabia ya uvivu hii ndio ambayo ningependa kutoa wito kwa wananchi wangu ndani ya mkoa wa Rukwa kuwa waache uvivu, mbona kuna mabinti na kina mama wanachapa kazi kule, hawakimbii wanapiga kokoto na wako wengi, lakini vijana wa kiume wanataka kupiga draft, kufanya vitu vyepesi vyepesi, hii tabia ningewaasa waiache,” alisema

Ameongeza kuwa kwa kufanya hivyo miradi hivyo wanakosa umiliki wa miradi hiyo na kuiona ni miradi isiyowahusu na hivyo kuwataka wananchi kujitokeza katika ufundi na vibarua ili kufanye kazi na kujipatia kipato na kuacha uvivu.

Ameyasema hayo alipotembelea ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Nkasi inayojengwa katika mji mdogo wa Namanyere wilayani humo akiongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa pamoja na wataalamu kutoka katika ofisi ya mkuu wa mkoa.

Katika ziara hiyo Mh. Wangabo amepongeza hatua iliyofikiwa katika ujenzi huo unaoendelea huku majengo yote saba ya hospitali hiyo yakiwa yamefikia katika hatua ya kupaua na kuzingatia ubora katika ujenzi huo huku vifaa vyote kwaajili ya ujenzi huo vikiwa tayari vimeshanunuliwa na kuwaasa kuwa hadi kufikia tarehe 30.6.2019 wahakikishe mafundi wanakabidhi majengo hayo kwaajili ya kuanza kutumika.

Mmoja wa vibarua anaetokea mkoa wa shinyanga kwa niaba ya wenzie alisema kuwa tangu wafike hapo wamekuwa wakilipwa vizuri na wanaona kuwa kazi zinakwenda sawa na hawana malalamiko yoyote huku fundi wao mkuu katika jengo la maabara alikiri kuwa vibarua wake anawatoa mkoa wa shinyanga na kuwa vijana waliopo katika wilaya ya Nkasi ni wavivu na walikuwa wakirudisha nyuma kasi ya kazi.

Awali akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa hospitali hiyo Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda alisema kuwa ujenzi huo unakwenda kwa awamu tatu na hadi kufikia tarehe 15.6.2019 awamu ya kwanza itakuwa imeisha na awamu ya pili ya kupaka majengo rangi pamoja na kuweka fremu za milango na madirisha tayari imeshaanza kufanyika na awamu ya mwisho ni kuweka marumaru kwenye majengo yote hivyo hadi kufikia tarehe 30.6.2019 ujenzi huo utakuwa umekamilika.

“Kwa zote hadi sasa tumeshatumia kama shilingi bilioni 1.15 na mpaka jana kweny akaunti tuna kama shilingi milioni 351 ambazo matarajio yetu ni kwamba zitakidhi shughuli za mradi kwasababu kwa upande wa mafundi wote wameshalipwa haki zao kitu ambaco kimebakia katika kununua ni masuala ya marumaru na kulipia aluminiam ya vioo na kumalizia kuwalipa mafundi wakaofanya kazi awamu ya pili, matarajio yetu fedha hiyo itakidhi mahitaji hayo,” Alimalizia.

Matangazo

  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAWEKEZAJI KUTOKA ZAMBIA WAVUTIWA NA BANDARI MKOANI RUKWA

    May 28, 2023
  • MRADI WA MAJI WAZINDULIWA KISA

    May 15, 2023
  • ZAHANATI YA MPONA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA YAZINDULIWA

    May 15, 2023
  • UPENDO, MAADILI NA FAMILIA IMARA MUAROBAINI WA UKATILI WA KIJINSIA

    May 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa