• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Uzinduzi Kampeni ya Tatu ya Polio

imewekwa Tar: August 31st, 2022

WATOTO 276,320 KUPATIWA CHANJO YA POLIO AWAMU YA TATU RUKWA

Na. OMM Rukwa

Mkoa wa Rukwa umepanga kutoa chanjo ya polio kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano kupitia kampeni ya nyumba kwa nyumba ambapo jumla ya watoto 276,320 wanatarajia kuchanjwa katika halmashauri zote nne.

Akifungua kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi jana (30.08.2022) mjini Sumbawanga, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga alisema lengo la mkoa ni kushika nafasi ya kwanza kitaifa kwa kuwafikia watoto wote waliolengwa kwenye kampeni hiyo ya awamu ya tatu.

“Jukumu letu ni kuhakikisha jamii inapata uelewa wa kutosha kuhusu chanjo ya polio ili washiriki kuunga mkono hatua itakayosaidia watoto wengi zaidi kupatiwa chanjo ndani ya muda uliopangwa. Kutunza watoto mwenye ulemavu ni jambo gumu hivyo tuwakinge watoto wetu ,” alisema Sendiga.

Mkuu huyo wa Mkoa alitoa wito kwa viongozi wa Serikali kuanzia wenyeviti wa vitongoji, mita na vijiji pamoja na wale wa madhehebu ya dini na mila kote mkoani Rukwa kuunga mkono kampeni hii kwa kuwezesha watoto wenye umri  chini ya miaka mitano wapatiwe chanjo hii ya polio.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Ibrahim Isaack alisema maandalizi ya kampeni ya polio awamu ya tatu itakayoanza Septemba 01 hadi 04  mwaka huu yamekamilika ambapo jumla ya dozi 276,320 zimepokelewa na kusambazwa katika halmashauri za Sumbawanga, Nkasi, Kalambo na Sumbawanga Manispaa.

Dkt. Isaack alibainisha kuwa jumla ya timu za wachanjaji 626 na Wasimamizi wapatao 168 zipo tayari kufanya zoezi la utoaji chanjo ya polio nyumba kwa nyumba ambapo wataalam wa afya wakishirikiana na wataalam toka Shirika la Afya Duniani (WHO).

Katika kampeni ya awamu ya pili ya Polio iliyomalizika mwezi Mei mwaka huu, mkoa wa Rukwa ulifanikiwa kushika nafasi ya tatu kitaifa kwa kuchanja watoto walio chini ya miaka mitano wapatao 268,362 kati ya lengo la mkoa watoto 217,674 sawa na asilimia 123.

Ugonjwa wa Polio unasababishwa na virusi vya Polio ambapo usipodhibitiwa mapema husababisha kupooza au ulemavu wa kudumu na hatimaye kifo.

Mwisho.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa