• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Viongozi wa dini Rukwa watahadharisha fujo siku ya Uchaguzi huku wakiliombea taifa.

imewekwa Tar: October 26th, 2020

Viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini mkoani Rukwa kupitia Kamati ya Amani ya Mkoa huo wamewatahadharisha wananchi hasa kundi la vijana kuachana na fikra za kuanzisha ama kuchochea fujo katika siku ya uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika kesho tarehe 28.10.2020.

Viongozi hao kwa nyakati tofauti wameyasema maneno hayo katika siku ya maalum iliyoandaliwa na Kamati hiyo ya Amani mkoani humo ili kuliombea taifa amani na kuuombea uchaguzi huo ufanyike kwa utulivu huku wakiwasihi wananchi kushiriki katika uchaguzi huo na kuondoka katika kituo cha uchaguzi mara tu baada ya kumaliza zoezi la kumchagua wanayemwona anafaa kuwaongoza kuanzia ngazi ya Kata, Jimbo na Nchi.

Wakati akitoa nasaha zake Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Mkoa wa Rukwa, Askofu Ambele Mwaipopo wa Kanisa la Kilutheri la Kiinjili Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Ziwa Tanganyika Mkoani Rukwa aliwaomba wananchi kuwachagua viongozi watakao ipeleka nchi ya Tanzania inapotakiwa kwenda na sio viongozi wanaoleta mizaha katika maendeleo ya nchi.

“Kwahiyo siku hiyo tupige kura tuwachague viongozi ambao wanatokana na kiti cha enzi cha Mungu mwenyewe, Mungu ameshajichagulia viongozi katika taifa hili, sisi tutathibitisha kwa kura zetu na Mungu apate kutukuzwa na abaki katika nchi ya Tanzania ipate kusonga mbele,” Alisema.

Naye Kiongozi wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) Mkoani Rukwa Sheikh Rashid Akilimali alisema kuwa vijana wa hivileo hawajawahi kushuhudia kutoweka kwa amani na kusahau kuwa kuna nchi za jirani ambazo waliwahi kushuhudia kutoweka kwa amani y ana matokeo yake walikimbilia nchini kwetu Tanzania kwaajili ya hifadhi na hivyo kuiomba serikali kuhakikisha vijana watakaosababisha fujo warudishwe katika mstari.

“Tarehe 28 tukapige kura ndio wito wangu, tuwachague viongozi ambao tutaona watatuletea maendeleo, tukawachague na mkuu wa mkoa anasema yule ambaye anaona hajakaa sawa kiroho akaenda kimwili tutamrudisha, mrudisheni kikwelikweli, asituvunjie amani yetu, mrudisheni, awe katika mstari barabara, tukapige kura asubuhi tumchague kiongozi tunayemtaka, kisha baada yah apo turudini kwenye makazi yetu,” Alisisitiza.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa rukwa mh. Joachim Wangabo aliyehudhuria katika dua hiyo maalum amesema kuwa kuna matayarisho ya kimwili na kiroho katika kuliendea zoezi la uchaguzi mkuu na kuongeza kuwa matayarisho ya kimwili yote yamekamilika ikiwemo Tume ya uchaguzi ya Taifa Pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama kujipanga vyema kukabiliana na wale ambao watakuwa wamekengeuka ambao hawataki kufuata maswala hayo ya kimwili.

“ lakini tupo hapa kuwaombea hao na kuiombea nchi yetu amani, sina shaka kabisa, Mwenyezi mungu amekuwa akitusikia, Ametusikia kwenye janga lile la Corona, sasa na hili pia atatusikia, imeandikwa kwenye maandiko matakatifu kwamba wakutanapo wawili wakimuomba yeye yupo na hapa tupo Zaidi ya wawili, tuko wengi viongozi hawa waliopo hap ani wawakili tu wa waumini wote,” Alisema.

Maombi hayo yalifanyika jana (26.10.2020) katika viwanja vya Shule ya Sekondari kizwite ikiwa ni kutimiza azma ya Kamati ya Amani mkoa kuliombea taifa kuwa na uchaguzi wa amani

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO POLIO

    September 15, 2023
  • HALI YA USALAMA KABWE NI SHWARI, KAZI IENDELEE

    September 12, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa