• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wafanyabiashara Lipeni Kodi Kwa Hiari

imewekwa Tar: September 14th, 2021


WAFANYABIASHARA RUKWA LIPENI KODI KWA WAKATI-

RC MKIRIKITI

 

Wafanyabiashara wa mkoa wa Rukwa wametakiwa kuwa na mtindo wa kulipa kodi kwa hiari ili kuwezesha serikali kupata mapato ya kutekeleza miradi ya maendeleo.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti jana (13.09.2021) wakati alipofungua semina ya utoaji elimu ya kodi iliyotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mjini Sumbawanga.

“Ni vizuri wafanyabiashara wote mkawa na utaratibu wa kulipa kodi kwa hiari badala ya kusubiri mivutano kwani serikali inategemea fedha hizo kwa ajili ya kutoa huduma kwa umma” alisema Mkirikiti.

Katika semina hiyo iliyowakutanisha wafanyabiashara mbalimbali wa mjini Sumbawanga, Mkirikiti aliwataka watumie pia fursa ya fedha zinazotolewa na serikali kwa miradi ya afya, shule na miundombinu ili washiriki  ujenzi wa miradi hiyo.

Mkirikiti aliongeza kusema serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuleta fedha nyingi za miradi ikiwamo Shilingi Milioni 750 za hii karibuni zilizotokana na tozo ya miamala ambazo zinakwenda kujenga vituo vitatu vya afya kwenye tarafa za mkoa wa Rukwa.

Mkuu huyo wa Mkoa alitaja vituo vya afya vitakavyojengwa kuwa ni  Mwazye ( Kalambo), Kate ( Nkasi) na Kipeta ( Sumbawanga) ambapo kila kimoja kimepatiwa Shilingi Milioni 250 kwa awamu ya kwanza mwezi Agosti mwaka huu.

“Ninapenda wafanyabiashara wa Rukwa muwe na taarifa za miradi na fedha zinazotolewa na serikali ili iwe chachu kwenu kujitokeza kutekeleza na kutoa huduma ili mpate fedha pia serikali ipate kodi badala ya kuachia miradi hiyo wafanyabiashara toka nje ya Rukwa” alisisitiza Mkirikiti.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi toka Mamlaka ya Mapato Tanzania Richard Kayombo alisema wapo mkoani Rukwa  kuelimisha walipa kodi juu ya umuhimu wa kulipa kodi kwa hiari na kusikiliza changamoto zao.

Kayombo aliongeza kusema TRA itaendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato bila mikwaruzano ambapo msingi mkubwa ni kutekeleza Agizo la Rais Samia Suluhu Hassan la kuona kodi inakusanywa kwenye mazingira rafiki sio kutumia nguvu.

Naye Anusisye Thomas mkandarasi wa ujenzi alitoa ombi kwa serikali ya mkoa kuwezesha wazabuni na wakandarasi wa ndani kupata kazi za miradi ya serikali ili wanufaike kiuchumi na kuwa na uwezo wa kuchangia maendeleo ya mkoa wa Rukwa badala ya kutumia wakandarasi wa nje.

Mwisho

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa