• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi 2,300 Wapata Chanjo ya UVIKO-19

imewekwa Tar: August 18th, 2021

WANANCHI 2,300 WAPATA CHANJO YA UVIKO-19 RUKWA: DKT.KASULULU

Serikali imebainisha mafanikio ya zoezi la kutoa chanjo ya kinga dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona (UVIKO-19) ambapo wananchi wapatao 2,300 tayari wamejitokeza kupata chanjo hiyo mkoani Rukwa tangu kuzinduliwa kwa zoezi hapo mwanzo mwa mwezi huu.

Hayo yamebainishwa leo (17.08.2021) na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye kituo cha Afya Halmashauri ya wilaya Kalambo. 

Mganga Mkuu huyo alisema takwimu zinaonesha tangu kuzinduliwa kwa zoezi la kutoa chanjo hapo Agosti 03 mwaka huu wananchi wengi kwenye wilaya tatu za mkoa wa Rukwa wameendelea kujitokeza ambapo jumla ya watu 2,300 wamekwishapatiwa chanjo kwa hiari kati ya dozi 20,000 zilizopokelewa mkoani.

Dkt. Kasululu akiwa kwenye kituo cha Afya Matai Wilaya ya Kalambo alitumia fursa hiyo kuendelea kuwasihi wananchi kuwa chanjo zinazotolewa na Serikali ni salama na kuwa zimefanyiwa tathmini mathalani hadi sasa kitaifa watu zaidi ya Laki Mbili tayari wamepata chanjo hiyo ya UVIKO 19 kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Afya.

“Kama Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amechanja, Mkuu wa Mkoa wetu Joseph Mkirikiti amechanja nami pia nikiwa Mganga Mkuu wa Mkoa nimechanja pia zaidi ya watu wengi tayari wamechanja hakuna haja ya kuogopa kuchanja chanjo hii ya UVIKO 19” alinukuliwa Dkt. Kasululu.

Alipoulizwa kuhusu changamoto kwenye zoezi hilo Dkt. Kasululu alibainisha kuwa Wilaya ya Kalambo bado kuna mwitikio mdogo ukilinganisha na halmashauri zingine kutokana na baadhi ya taarifa za upotoshaji wa baadhi ya watu.

Awali akifungua kampeni ya usawazishaji wa vikope kwa wananchi wenye matatizo mbali mbali ya macho Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryoba aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aliwasihi wananchi wa Wilaya ya Kalambo kuendelea kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO 19 huku wakichukua tahadhari zingine.

Mkuu huyo wa Wilaya alibainisha kuwa pamoja na kuchukua jitihada zingine za kujikinga na UVIKO 19 ni budi wananchi wakaendelea kumwomba Mungu aliepushe Taifa letu na janga la Corona.

“Tuendelee kumwomba Mungu atuepushe na ugonjwa huu wa Corona na Tanzania iendelee kuwa nchi salama huku tukizingatia ushauri wa wataalam wa afya” alisema Waryoba.

Mkoa wa Rukwa ulipokea dozi 20,000 za chanjo UVIKO 19 ambapo awali ilitenga vituo 11 vya kutoa chanjo lakini kutokana na ukubwa na mtawanyiko wa watu imelazimu kuongeza vituo pia kutumia huduma vikoba (mobile clinic) ili kuwafikia wananchi wengi waliopo mbali na vituo vya afya.

Mwisho.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa