• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi 638,979 Rukwa Wahusiwa kushiriki kupiga kura Uchaguzi Mkuu tarehe 28 Oktoba

imewekwa Tar: September 22nd, 2020

Mkuu wa mkoa wa Rukwa mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi 638,979 wa vijiji vyote 339, Mitaa 167, Kata 96, Tarafa 16, Halmashauri 4 na Wilaya 3 Mkoani Rukwa walioandikishwa kwaajili ya kupiga kura, kujitokeza katika kupiga kura katika uchaguzi mkuu utaofanyika siku ya Jumatano ya tarehe 28 mwezi Oktoba mwaka huu ili kuwachagua Madiwani, Wabunge Pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Aidha, Mh. Wangabo ametumia nafasi hiyo kuwakumbusha wakulima kuwa katika kipindi hiki cha Kampeni wasisahau kuandaa mashamba yao kwaajili ya msimu wa kilimo wa mwaka 2020/2021 na kusisitiza kuwa wananchi wasiegemee sana siasa wakasahau Maisha ya kawaida ambayo ni kilimo kwa wananchi wengi wa mkoa wa Rukwa.

“Wakati huo huo vyote lazima viende Pamoja na maandalizi ya kilimo, si mvua karibu zinanyesha, ni lazima watu wakaandae mashamba yao, tusiegemee sana siasa tukasahau pia kuna Maisha ya kawaida kwetu sisi ni kilimo, kwahiyo ni lazima tuandae mashamba mapema, uchaguzi unapopita mvua zikinyesha tunakwenda kupanda, mvua za kwanza ni za kupandia, kwahiyo vyote tuvibebe, tumeelewana,” Alisistiza.

Mh. Wangabo ameyasema hayo alipotembelea miradi ya Lipa kulingana na Matokeo (EP4R) na Miradi ya Afya na Usafi wa Mazingira (SWASH) inayotekeleza ujenzi wa madarasa na vyoo vya wananfunzi kwa shule za msingi na Sekondari Wilayani Kalambo ambapo wilaya hiyo imepokea jumla ya Shilingi 529,679,504 kwa mwaka huu wa fedha ili kutekeleza miradi hiyo.

Awali wakati akisoma taarifa ya miradi hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo, Afisa Mipango wa Halmashauri hiyo Eric Kayombo alisema kuwa Shilingi 353,900,000 ilipokelewa katika shule saba za msingi kwaajili ya ujenzi wa madarasa na vyoo na Shilingi 175,776,504 ilipokelewa katika shule nyingine 7 za msingi kwaajili ya ujenzi wa vyoo.

“Mheshimiwa Mkuu wa mkoa utekelezaji wa miradi hii umeanza mwaka huu wa fedha 2020/2021 badala yam waka 2019/2020 hii ni kutokana na halmashauri kupokea fedha za miradi mwishoni mwa mwaka wa fedha 2019/2020 na kufanya kuvuka mwaka na kuanza kutekeleza mwaka huu wa fedha, Miradi ya EP4R ipo katika hatua za msingi na miradi ya afya na usafi wa mazingira ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji,” Alisema.

Mh. Wangabo ametoa miezi miwili kwa halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kuhakikisha wanamaliza miradi hiyo kwa shule za msingi na sekondari ili kuimarisha miundombinu ya shule hizo ambazo iradi hiyo inatekelezwa ikiwemo shule ya sekondari ya Wasichana Matai ambayo inatarajiwa kuanza kupokea wananfunzi kuanzia mwaka 2021.

Matangazo

  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAWEKEZAJI KUTOKA ZAMBIA WAVUTIWA NA BANDARI MKOANI RUKWA

    May 28, 2023
  • MRADI WA MAJI WAZINDULIWA KISA

    May 15, 2023
  • ZAHANATI YA MPONA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA YAZINDULIWA

    May 15, 2023
  • UPENDO, MAADILI NA FAMILIA IMARA MUAROBAINI WA UKATILI WA KIJINSIA

    May 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa